WAZAZI WATAKIWA KUACHA KUWAAGIZA WATOTO MAENEO YA MGODI WA GGM

Share it:
Watoto wakiwa kwenye shimo la kutupia uchafu ndani ya mgodi wa dhahabu wa Geita (GGM)wakiogota vyuma chakavu vinavyokuwa vimetupwa na mgodi huo.

Afisa mahusiano wa mgodi wa GGM .Mussa Shunashu akionesha maeneo ambayo ni hatarishi kwenye mgodi huo.

Eneo la kutupia taka kwenye mgodi wa dhahabu wa Geita.

Bi,Sarah Kajoro akiwa kwenye masikitiko kutokana na mtoto wake kushindikana na kujikuta akielekea maeneo ya mgodini.

Mzazi akijaribu kumwazibu mwanae kutokana na kuwa na tabia ya kwenda kwenye maeneo ya mgodi wa GGM.

Mwenyekiti wa mtaa wa Kompaundi ,Edgha Onyango akielezea hatua ambazo wameendelea kuzichukua dhidi ya wazazi ambao wamekuwa wakiwaruhusu watoto wao kwenda maeneo ya mgodini.

Mkuu wa wilaya ya Geita,Mwl Herman Kapufi akikemea vikali tabia ya baadhi ya wazazi kuendelea kuwatumikisha watoto kuwa watafutaji badala ya wao kutafuta.



Kumekuwepo na wimbi kubwa la watoto kuingia kwenye maeneo ya mgodi wa dhahabu wa Geita(GGM),kwa madai baadhi yao wamekuwa wakitumwa na wazazi wao  na walezi kwa ajili ya kuokota vyuma chakavu na mawe ya dhahabu maarufu kwa jina la magwangala hali ambayo inaweza kusababisha  kutokea kwa hatari kwa watoto hao kutokana na maeneo mengi kutokuwa salama.

Hali hiyo inatokana na wazazi na walezi kushindwa kufuatilia kwa umakini muda wa  wengi kushindwa kujali masomo na kujikuta wakitumia njia za panya kuingia kwenye mgodi huo uliopo wilaya ya geita kata ya mtakuja mjini humo.

Wakizungumza  na mtandao huu  kwenye eneo la kutupia uchafu ndani ya mgodi huo baadhi ya watoto hao wamesema kuwa wamekuwa wakiingia kwa ajili ya kuwinda wanyama pori ambao wanapatikana kwenye maeneo ya mgodi huo.

“Sisi tunaingia humu kwa nia tu ya kuwinda wanyama pori wala sio masuala ya kuogota vyuma na mangwangala”Alisema mmoja wa watoto hao.

Afisa mahusiano wa mgodi huo bw,Mussa Shunashu amewashauri watoto hao ambao wamekuwa wakiingia kwenye maeneo hayo kuachana na tabia hiyo na badala yake watumie muda huo kujisomea kwani kufanya hivyo wanaweza kujikuta wanaingia kwenye matatizo kutokana na maeneo mengi ya mgodi kuwa hatari kwa maisha ya watoto hao.

Baadhi ya wazazi ambao wamezungumza na mtandao huu umesikitishwa na kitendo cha watoto kwani wengi wao wamekuwa wakitoroka nyumbani pasipo wazazi kujua wanakwenda wapi.

Mwenyekiti wa mtaa wa kompaundi  ambao unauzunguka mgodi huo,bw ediga Onyango,amewataka walimu wakuu wa shule za msingi kutoa taarifa kwenye uongozi wa mtaa pamoja na wazazi kuachana tabia ya kuwaagiza watoto kwenye maeneo ya mgodini.

Aidha  mkuu wa wilaya ya Geita Mwl,Herman Kapufi amewaonya wazazi wenye tabia hizo na kwamba hatua  kali zitachukuliwa kwa mzazi ambaye hatagundulika anamuagiza mtoto wake kwenye maeneo ya mgodi wa GGM.

Takwimu za watoto ambao wamekuwa wakiingia mgodini wa ggm zimeendelea kupanda ambapo kwa wastani kila mwezi  watoto sitini(60) wenye umri wa miaka sita na saba hadi 10 wameendelea kuingia kwenye maeneo hayo hatarishi.

Share it:

habari

Post A Comment: