WATU WENYE UALBINO BADO WANAKABILIWA NA TATIZO LA SARATANI YA NGOZI PAMOJA NA SWALA LA UNYANYAPA KATIKA JAMII WANAZO ISHI.

Share it:




Wajumbe na mgeni Rasmi katika uzinduzi wa program ya uwezeshaji ,msaada wa kisaikolojia,elimu na vifaa vya shule kwa watu wenye ualbino ambapo ulifanyikia katika ukumbi wa Yohana Memoriol center.



Baadhi ya wajumbe wakifatilia kile ambacho kilikuwa kikiendelea meza kuu.

Mratibu wa Briggitte Alfred Foundation Stanley Mosha,akitoa neno la shukrani kwa Mgodi wa Dhahabu wa GGM kwa kujitolea kutoa msaada wa fedha ili kufanikisha Program hiyo.



Mkurugenzi Mtendaji wa NELICO,Paulina Alex akifafanua namna ambavyo kumekuwepo na changamoto za watu wenye ualbino kukosekana kwa matibabu ya kansa pamoja na kunyanyapaliwa katika familia na jamii zinazowazunguka.

Makamu wa Rais wa mgodi wa dhahabu wa GGM,Saimon Shayo akielezea namna ambavyo wachimbaji wanatakiwa kuachana na imani ambazo si nzuri kwamba ambazo zimekuwa zikisababisha mauwaji ya watu wasio na hatia. 

Mkuu wa Wilaya ya Geita,Herman Kapufi akisisitiza namna ambavyo serikali imejipanga kuweka usalama wa kutosha kwa watu wenye ualbino hususani katika wilaya anayoisimamia.

Mfano wa Hundi ya Milioni 30,ikikabidhiwa kwa mgeni rasmi pamoja na Mkurugenzi wa Nelico na Mratibu wa Briggitte Alfred,ambazo zimetolewa na mgodi wa dhahabu wa GGM.






Suala la Unyanyapaa pamoja na ugongwa wa saratani ya ngozi kwa watu wenye ulemavu wa ngozi (albinism) ni tatizo ambalo limeendelea  kuwafanya kuishi kwa mashaka katika familia na jamii zinazowazunguka.

kauli hiyo imetolewa na mkurugenzi wa shirika la kusaidia watoto na watu wenye ulemavu (NELIKO) Paulina  Alex wakati wa uzinduzi wa mradi kuwajengea uwezo, na kutoa elimu kuhusu afya na namna ya kujilinda kwa watu wenye ulemavu wa ngozi albino.

uzinduzi huo umefanyika katika ukumbi wa  Yahana Memorial  Centre uliopo mjini Geita.

Paulina amesema Ugongwa wa saratani ya ngozi  kwa wenye ulemavu wa ngozi (albino) ni kikwazo kikubwa sana na kwamba kwa wilaya ya Geita kuna wagonjwa watano (5) wanaohitaji msaada wa matibabu kutokana na hali zao kuwa mbaya.

“katika wilaya  yako ya Geita kuna watu wenye albinism watano ambao ni wagonjwa wa kansa wanahitaji msaada mkubwa sana na kuna watu wenye albinism wawili ambao wao imefikia kasa yao kwenye hatua ya nne ni sikitiko kidogo swala hili tujaribu kulipa
kipaumbele ili kuwasaidia wenzetu changamoto nyingine ni swala la unyanyapaa katika familia zetu bado ni tatizo”alisema Paulina

Mwenyekiti  wa Tas  wilaya ya Geita, Lazaro Malendeja amesema kuwa maradhi ya saratani yamekuwa ni adui mkubwa sana ambae anasumbua watu wenye ualbino na hii ni kutokana na changamoto kubwa ya kukosekana kwa huduma ya afya katika upande wa saratani kwani mara nyingi wamekuwa wakienda jijini Dar es salaam kutibiwa hivyo ameomba kwa serikali kuona umuhimu wa kuleta kitengo cha huduma ya saratani katika hosptali zilizopo mkoani hapa.

Naye makamu wa rais  wa mgodi wa  dhahabu wa Geita (GGM)  Simoni Shayo amewataka wachimbaji  kuacha imani potofu ya kwamba mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi (albino)  yanasababisha upate utajiri huku walengwa wa mradi huo wakipongeza kwa kupewa  msaada huo.

Akizungumza wakati wa kufunga uzinduzi huo kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Geita,mkuu wa wilaya ya Geita mh Herman Kapufi amesema  serikali mkoani hapa  imejipanga kuwakamata na kuwachukulia hatua kali  watu ambao wamekuwa wakitishia maisha ya watu wenye ulemavu wa ngozi.

kampuni ya kuchimba madini ya dhahabu ya Geita (GGM) mkoa wa Geita katika kuunga mkono juhudi za kupinga  mauwaji  ya watu wenye ulemavu wa ngozi imetoa hundi ya kiasi cha sh milioni thelathini (30) kwa ajili ya kuwezesha jambo hilo, huku wakiomba fedha ziwafikie     walengwa.

Imeandaliwa na Joel Maduka.
Share it:

habari

Post A Comment: