Afisa Madini wa Mkoa wa Geita Ally Said Ally akielezea juu ya leseni ya mgodi huo
Zaidi ya
wachimbaji mia moja (100) wa kata ya Lwamgasa Wilayani Geita wamevamia kwenye
maeneo ya Mgodi wa Buckreef na kuanza shughuli za uchimbaji kwa madai kuwa
mwekezaji amemaliza muda wake ana hataki kuwapatia fidia ya maeneo yao.
Akizungumzia juu ya tatizo ambalo limepelekea wachimbaji
kuvamia Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi
CCM Kwenye kata Hiyo Edward Kiswaga
,amesema kuwa kuna watu ambao walitathiminiwa na walitakiwa kulipwa na kwamba
takribani miaka minne wamekuwa wakizungushwa juu ya kupatiwa fidia zao.
“Tuliwai
kuja na Mheshimiwa Kalemani wakaahidi kwamba watajenga barabara na kutoa huduma
kwa wanajamii wa Lwamgasa lakini
nimekuwa nikifuatilia kwa Mheshimiwa Minda na nina wauliza kwa nini hamtekelezi
ahadi zenu wamekuwa wakisema Mkurugenzi yupo Canada huku kuna watu ambao tayari
wameshatathiminiwa wanatakiwa kulipwa fedha zao”Alisema Kiswaga
Kutokana na
madai ya kutokulipwa fidia ya maeneo yao Meneja wa Mgodi wa Buckreef , Peter
Zichovu amesema kuwa walikuwa na mpango wa kuwalipa watu hao lakini tatizo
kubwa ambalo lilionekana ni watu kuongezeka na kwamba walikuwa wana mpango wa
kufanya tathimini na kuwalipa watu hao ambao wamekuwa na madai ya fedha zao.
Kutokana na
maelezo hayo Mkuu wa Wilaya ya Geita Mwl Herman Kapufi ambaye alikwenda kutatua shida hiyo kwa wananchi amesema kuwa tarehe
15 watakutana yeye na naibu Waziri kwenye eneo hilo na kwamba amewapa
wachimbaji hao siku tatu (3) kufanya shughuli za uchimbaji na baada ya hapo wayaachie
maeneo hayo hadi pale uwamuzi utakapofikia wa maeneo hayo.
Eneo la Buckreef lina leseni ya uchimbaji Mkubwa
na kwamba leseni hiyo inamilikiwa ubia
kati ya shirika la madini la Taifa Stamico pamoja na kampuni ya Tanzamu na
kwamba leseni hiyo inadumu miaka kumi (10) na kwamba imekwisha kumalizika
lakini tayari wamekwisha fanya taratibu za kubadilisha (kulinew) leseni hiyo ingawa
bado haijawekewa saini na Waziri mwenye dhamana.
IMEANDALIWA NA MADUKA ONLINE
|
Post A Comment: