MBUNGE WA BUKOMBE ASISITIZA MATUMIZI BORA YA FEDHA ZA MIKOPO KWA WAJASIRIAMALI

Share it:
Mbunge wa Jimbo la Bukombe,Doto Biteko akizungumza na wananchi(PICHA NA MAKTABA YA MADUKA ONLINE)

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge,Ajira na Watu wenye ulemavu Jenista Mhagama akizungumza na baadhi ya wajasiriamali wakati wa shughuli ya kuzindua utoaji wa mikopo yenye thamani zaidi ya milioni mbili Mkoani Geita.


Mheshimiwa Doto akimsikiliza waziri wa Nchi ofisi ya waziri Mkuu sera,bunge,ajira na watu wenye ulemavu Jenista Mhagama.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge,Ajira na Watu wenye ulemavu Jenista Mhagama,akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa Mkoa wa Geita na wabunge wa majimbo yaliyopo Mkoani humo.

(Na Joel Maduka. )
Mbunge wa Jimbo la Bukombe Doto Mashaka Biteko,amewaomba wananchi ambao wamepatiwa mikopo kutoka  baraza la utendaji la uwezeshaji wananchi kiuchumi kutumia fedha hizo kwa manufaa ikiwa ni pamoja na kuhakikisha wanainuka kiuchumi kutoka hapo walipo kwenda juu zaidi.

Rai hiyo ameitoa wakati wa shughuli za kukabidhi hundi kwa wajasiriamali 3824 ambao wanajumuhisha mikoa mine ya kanda ya ziwa.
Mheshiwa Doto,alisema kuwa ni vyema Mikopo ambayo wamepatiwa ikageuka kuwa nuru kwenye maisha yao na sio kuleta shida hali ambayo inaweza kupelekea wakaanza kukimbia hata pindi wanapoona magari ya viongozi wa serikali wakiwemo wakuu  wa Wilaya.

“Kwa wale ambao watapokea mikopo hii leo(jana) wapo pia wananchi wa wilaya ya  Bukombe  nimeambiwa kuwa jumla wapo 422 kati yao 322 ni wakina mama kwa hiyo utaona zaidi wakinamama wamepata fursa hii na mimi niseme tu mheshimiwa waziri sisi wananchi wa Bukombe tunakushukuru sana lakini niwaomba wananchi tusikimbiane baada ya kuwa tumekopa hisiwe kukopa furaa kulipa ni majanga”Alisema Doto.

Doto aliendelea kuwaomba wananchi hao baada ya mwaka wanapokutana basi kila mmoja awe anajambo ambalo amelipata kutokana na kupatiwa mikopo hiyo.

Aidha kwa upande Mwingine Doto amemshukuru Mheshimiwa, Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu  Jenista Mhagama  kwa kuendelea kutenda kila jambo ambalo amekuwa akilisema.

Naye Mbunge wa Nyang'hwale  Hussen Kasu ametumia nafasi hiyo  kuziomba taasisi za mikopo kuelekeza nguvu za mikopo kwenye jimbo lake kwani pia kuna watu ambao wanauitaji wa kukopa.

Hata hivyo kwa upande wake , Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu  Jenista Mhagama  amewasisitiza wananchi kuchangamkia fursa ya mikopo kwani hayupo mtu ambaye ameendelea bila ya kukopa hivyo ni vyema wakatumia njia hizo kama sehemu ya kujikwamua na kujiinua kiuchumi.

Vikundi vya Wajasiriamali waliofaidika ni kutoka Mkoa ya Kagera,Geita,Simiyu,Mara na Mwanza na jumla ya wajasiriamali 3824 kati yao wanawake ni 2,161 sawa na asilimia 57.Jumla ya Mikopo iliyotolewa kwa Wajasiriamali  ni zaidi ya Bilioni mbili.





Share it:

BIASHARA

Post A Comment: