AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA WIZI WA KUTUMIA SILAHA.

Share it:





JESHI la Polisi Wilayani Bukombe Mkoani Geita limemfikisha Mahakamani Abdulazizi Mohamed mkazi wa Runzewe kwa kosa la unyang’anyi wa kutumia Silaha kisha kupora Pikipiki.

Mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi ,Mwandamizi wa Mahakama ya Wilaya ya Bukombe Gabriel Kulwijira mwendesha mashitaka wa Polisi Lazaro Mhegele mahakamani hapo alisema mshitakiwa Abdulazizi anashitakiwa kwa kosa la unyang’anyi wa kutumia silaha kinyume na kifungu Na 287 A cha sheria ya kanuni ya adhabu sura  ya 16 iliyofanyiwa marejeo 2002 na kufanyiwa marejeo tena kwa sheria Na 3/2011.

Mhegele alisema mshitakiwa abdulazizi alitenda kosa hilo septemba 11, 2016 majira ya saa 2.30 usiku katika kijiji cha Busonzo  akiwa na mwenzake waliiba Pikipiki yenye namba  za usajili MC 622 BKB yenye thamani ya Sh.1950,000 mali ya Omari Shaban mkazi wa kijiji cha Runzewe.

Akizungumzia mazingira ya Tukio hilo mwendesha mashitaka huyo wa polisi alisema mshitakiwa  na mwezake walikodi Bodaboda hiyo iliyokuwa ikiendeshwa na dereva Hamis Charles (20) ili awapeleke kijiji cha Busonzo kwa mganga wa kienyeji majira ya saa 11 jioni akawapeleka na ilipofika saa 2.30 usiku walimpigia simu awafuate huko kwa sangoma akawafuata na waliponza kurudi walipofika njiani wakamwambia asimame akasimama kisha wakaanza kumshambulia kwa mapanga hadi akazirahi nao wakafikiri kuwa ameshapoteza maisha wakachukua pikipiki hiyo na kutokomea kusikojulikana.

Alisema mungu si Athumani dereva bodaboda huyo alizinduka na akapata fahamu akajikongoja kwa nguvu za wasamaria wema hadi kituo cha Polisi Runzewe akaripoti kwani kati ya hao waporaji alimtambua Abdulazizi Mohamed akawapeleka hadi anapofanyia kazi zake  mjini Runzewe na kisha uwamuzi wa kukamatwa ndipo ulifanyika


Mnamo septemba 27, 2016 alifikishwa mahakama ya wilaya na kusomewa mashitaka yanayomkabili mshitakiwa alikana shitaka ndipo Hakimu Gabriel Kulwijira aliiahirisha kesi hiyo hadi oktoba 10 ,2016 itakapo tajwa tena.

Na Peter Makunga 
Share it:

matukio

Post A Comment: