SERIKALI IMEWATAKA WATUMISHI WA IDARA MBALI MBALI MKOANI GEITA KUTUMIZA WAJIBU WAO.

Share it:



Naibu waziri wa Nchi, Ofisi ya Raisi tawala za mikoa na serikali za mitaa (Tamisemi) Mh,Seleman  Jafo,akitoa maagizo kwa watumishi Wilayani Mbongwe Mkoani Geita.



GEITA:Naibu waziri wa Nchi, Ofisi ya Raisi tawala za mikoa na serikali za mitaa (Tamisemi) Mh,Seleman  Jafo amewataka watumishi wa idara mbalimbali wilayani Mbogwe mkoani Geita kutimiza wajibu wao katika maeneo yao ya kazi kwa kuwatumikia wananchi wenye imani kubwa na serikali ya awamu ya tano katika kuwaletea mabadiliko.

 Hayo ameyasema  wakati akizungumza na watumishi wa halmashauri ya wilaya ya Mbogwe katika ukumbi wa Casablanca,amesema watumishi wengi wamekuwa wakifanya kazi kwa mazoea hali inayokwamisha utendaji kazi wa serikali na  kuwataka kubadilika kwa kufanya kazi kwa kutumia taaluma zao na  kutimiza majukumu kwa kuwatumikia wananchi.

Katika hatua nyingine Mh,Jafo amesema wakuu wa idara mbalimbali nchini wamekuwa wakichangia kuuwa vipaji vya watumishi kwa kushindwa kushughulikia matatizo yao kwa wakati hali inayoshusha uwezo kwa watumishi kujituma kufanya kazi.

“Morali ya wafanyakazi inatokana na mambo mengi jambo la kwanza ni kushughulikia madai ya watumishi, watu maeneo mengine wanapandishana madaraja kwa upendeleo na maeneo mengine inaenda mbali mwingine hampandishi daraja paka atoe rushwa na rushwa mbaya kuliko zote ni rushwa ya Ngono yani mtu hampandishi mtu daraja paka amdhalilishe utu wake na thamani yake naomba niwasihi haya mambo hatupendi yatokee Bukombe na nyinyi wakuu wa idara fanyeni kazi kwa uwadilifu kila kitu kikae sawa”Alisema Jafo

Aidha Mh,Jaffo amewataka wakuu wa Idara na watumishi wengine kujiamini wakati wa kazi kwa kutenda haki kwa kila mmoja hasa katika kuwatumikia wananchi na  kuacha majungu sehemu zao za kazi ili kuleta mabadiliko na ufanisi katika kazi.




Share it:

habari

Post A Comment: