BODABODA SERIKALI YAWATAMBUA KUWA NAYO NI AJIRA WAWEZESHWA

Share it:
Mkuu wa wilaya ya Mbongwe Martha Mkupasi akifafanua juu ya mafunzo ya madereva boda boda.
Boda boda kazini.



Serikali Wilayani Mbogwe Mkoa wa Geita imeanza kuwatambua  vijana wanaojiajili  hususani  waendesha Bodaboda kwa kuwapa Elimu itakayowawezesha  kupokea na kuzitumia Fulsa mbalimbali zitolewazo  kwa vijana.
 
Akizungumza na Maduka online Mkuu  wilaya  ya Mbogwe Martha Mkupasi alisema wamekuwasudia kutoa elimu kwa waendesha boda boda kutokana na kwamba hawana mabasi ya kutosha.
“elimu ambayo tunatoa ni vyema wakajiunga kwenye vikundi ili tuweze kuwatambua na halmashauri itasaidia kuwasajili vijana hao”alisema Mkupasi.

Hatua ya Serikali wilayani hapa kuwapatia elimu vijana hao waendesha Boda boda ni kutokana na uelewa wao mdogo hali ambayo wamekuwa wakikimbizana na Polisi sanjari na kukosa sifa za kuaminiwa na kutambuliwa.

Mkupasi ametoa wito  kwa jamii kutambua kuwa boda boda ni ajira inayosaidia vijana wengi kujikwamua.

Bodaboda serikali imewatambua na imewathamini ni juu yenu kutii ili mpate kuondokana na adha ya kukimbizana na Polisi sambamaba na kuondokana na Umaskini.

Imeandaliwa na Joel Maduka.

Share it:

habari

Post A Comment: