WANANCHI WILAYANI GEITA WATAKIWA KUTUMIA VYOO BORA NA KUNAWA MIKONO PINDI WANAPOTOKA CHOONI.

Share it:



Mifano ya mashimo ya vyoo bora

Vyoo bora kikiwemo choo ambacho mlemavu anaweza kukitumia kwa wepesi zaidi.

Mfano wa choo Bora kilichokamilika.


Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya Ali Kidwaka akipewa maelezo na mtaalam wa ujenzi wa vyoo bora.

Maelezo kutoka kwa wataalam tofauti juu ya ubora wa vyoo yakiendelea.

Mwandishi wa habari wa ITV,Rose Mweko akinawa mikono baada kutoka chooni.

Rose Mweko akitoka chooni.
Dr Hamis Marebo akimkaribisha Mgeni rasimi kuzungumza na wananchi juu ya swala matumizi ya vyoo na kunawa maji pindi wanapotoka chooni.


Muonekano wa baadhi ya vyoo visivyo bora.


Moja kati ya vyoo duni.

Dr Marebo akiangalia choo ambacho kimekoswa maitaji madogo kukifanya kiwe Bora

Mtafiti wa  Taasisi ya magonjwa  ya binadamu Bi, Yolanda Mbatia,Akimkabidhi mkurugenzi hati ya kituo kilichozinduliwa cha mafunzio ya vyoo bora

Ali Kidwaka,akionesha mfano ambavyo wananchi wanatakiwa kufanya pindi wanapotoka chooni.
Mkurugenzi Kidwaka akifafanua jambo kwa wananchi.

Dr Marebo akitoa Elimu kwa wananchi namna wanavyotakiwa kuwa mabarozi wema katika matumizi sahihi ya vyoo.

Mtafiti wa  Taasisi ya magonjwa  ya binadamu Bi, Yolanda Mbatia,Akielezea mafanikio waliyoyapata tangu kuanzishwa mradi wa vyoo bora.


GEITA:Wananchi katika halmashauri ya wilaya ya Geita,wametakiwa kuwa na mwitikio wa kutumia vyoo bora na kunawa mikono wakati wote pindi wanapotoka Chooni.

Hayo yamesemwa na mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya,Ali Kidwaka wakati wa zoezi la kukabidhiwa kituo cha mafunzo ya vyoo bora katika kata ya Katoma .


Kidwaka ,amesema kuwa tangu mwaka 2014 matumizi ya kutumia vyoo bora na kufata na unawaji wa mikono kwa   wananchi pindi wanapotoka chooni  asilimia zimeongezeka hadi kufikia 67 paka asilimia tisini ya sasa na bado jitihada zinaendelea kufanyika katika kuakikisha wananchi wanatumia vyoo bora ili kuepukana na magonjwa ya mlipuko ambayo yanaweza kutokea kutokana na kutokutilia maanani matumizi sahihi ya vyoo.

“Tunatambua kuwa matumizi sahihi ya vyoo ni muhimu kwa kila mwananchi ili kuepukana na magonjwa ambayo yanaweza kutishia kuondoa uhai wetu hivyo ni vyema kwa kila familia kuwa na choo bora na kukitumia.”alisema Kidwaka.

kwa upande wake, mtafiti wa  Taasisi ya magonjwa  ya binadamu Bi, Yolanda Mbatia,amesema kuwa lengo la kuja kuzindua mradio huo wa vyoo bora ni kutokana na hapo nyuma katika kata hiyo watu wengi walikuwa wanapata magonjwa yanayotokana na kinyesi cha binadamu.

Afisa afya wa  wilaya ya Geita,Nesfori Sungu,amesema kuwa kulingana na maelekezo ya mkuu wa wilaya kila mwananchi anatakiwa kuwa na choo ifikapo tarehe 30 mwezi wa  Tisa.

“Ni kila mwananchi anatakiwa kuwa na choo bora  na ifikapo tarehe 30 mwezi huu kama ambavyo mkuu wa wilaya alivyoagiza.”alisema Sungu
.

Hata hivyo wananchi wa kata  ya Katoma wameiomba serikali kupitia mradi wa vyoo bora kuona uwezekano wa kupunguza gharama za utengenezaji wa vyoo hivyo.

Imeandaliwa na Joel Maduka.
Share it:

habari

Post A Comment: