HALMASHAURI YA MBOGWE YAFUNGA MKATABA WA UJENZI WA OFISI MAKAO MAKUU MAPYA.

Share it:




















GEITA:Halmashauri Ya Mbogwe Yafunga Mkataba Wa Ujenzi Wa Ofisi Makao Makuu Mapya.

Halmashauri Ya Wilaya Ya Mbogwe Mkoani Geita Imeingia Mkataba Wa Ujenzi Wa Jengo La Ofisi Za Halmashuri  Zinazotarajiwa Kujengwa Katika Kijiji Cha Bwelwa Kata Ya Mbogwe.

Halmashauri Imesaini Mkataba Huo Na Kampuni Ya M/S  C.F Builders L.T.D  Ya  Jijini Mwanza .Mkataba Huo Utatekelezwa Kwa Miaka Mitatu 2016/2019 Na Utagharimu  3,994,947,386.10

Akiongea  Wakati Wa Kusaini Mkataba  Huo Mkurugenzi Mtendaji Wa Halmashauri Elias Kayandabila Alisema Wamefikia  Hatua Nzuri Na Ujenzi Utaanza Muda Wowote Na Itakuwa Fursa Kwa Wakazi Wa Mbogwe Kupata Ajira Za Muda Mfupi.

Vile Vile Mkurugenzi Kayandabila  Amesema Ujenzi Huo Utajengwa Kwa Awamu Kutokana Na Upatikanaji Wa Fedha Na Ameiomba Serikali Kuu Kuipa Kipao Mbele Halmashauri Kwa Kuwa Ofisi Zinazotumika Kwa Sasa Haziko Rafiki Kiutendaji Kwani Mazingira Yamechakaa Na Hayatoshelezi Wtumishi Wote.

Diwani Wa Kata Ya Mbogwe Sizya Nsika Amesema Amefurahi Kwa Hatua Iliyofikiwa Ya Kutia Saini Kwani Jambo Hilo Amelisubiri Kwa Muda Mrefu Lakini Utekelezaji Wake Ulikuwa Unalegalega .

Sizya Ametoa Shukrani Za Pekee Kwa Mkurugenzi Mtendaji Elias Kayandabila Kwa Kutilia Mkazo Suala Hili Muhimu.

Ujenzi Unaoenda Kuanza Utapelekea Viwanja Vya Halmashauri Vilivyopimwa   Kuuzika Baada Ya Kukosa Wateja Kwa Muda Mrefu.Viwanja Hivi Vilipimwa Kwa Mkopo Kwa Makubaliano Vikiuzika Mkandarasi Atalipwa Lakini Ilishindikana Baada Ya Wateja Kukosekana Na Kuingiza Halmashauri Katika Mgogoro Na Mkandarasi.

Ujenzi Huu Unarudisha Matumaini Kuwa Viwanja Vitauzika Sasa Kwani Watu Wengi Walikuwa Wanasubiri Ujenzi Kuanza Ili Kujiaminisha Kuwa Makao Makuu Ya Wilaya Ya Mbogwe Yatakuwa Mbogwe.


Imeandaliwa Na Peter Makunga
Share it:

habari

Post A Comment: