BUKOMBE:WAKULIMA WATAKIWA KUANZA KUANDAA MASHAMBA.

Share it:
Wakulima wakiwa katika uwandaaji wa shamba moja kati ya mashamba yaliyopo wilayani Bukombe.


Shamba la mboga mboga likionekana likiwa limestawi .







GEITA:Afisa Kilimo Umwagiliaji Na Ushirika Wilaya Ya Bukombe Mkoani  Geita, Joseph Machibya Amewataka Wakulima Wa Mazao Ya Chakula Na Biashara Kuanza Kupanda Mbegu Kwa Kutumia Mvua Zinazoendelea Kunyesha Ili Kuendasambamba Na Msimu Wa Kilimo  Wa Mwaka 2016/17

Machibya Amesema Kwa Mujibu Wa Watabiri Wa Hali Ya Hewa, Mvua Hizo Ni  Chache Katika Ukanda Wa Ziwa Victoria Hivyo Kila Mkulima Anapaswa Kuanza Kupanda Mazao Yake Kwa Kutumia Mvua Hizo Ili Kuenda Na Msimu Na  Kuongezeka Kwa Uzalishaji Wa Mazao .

 Ameendelea Kufafanua Kuwa  Wataalamu Wa Kilimo Wilayani Humo Wako Tayari Kushirikiana Na Wakulima Katika  Kutoa Elimu Ili Kuongeza Uzalishaji Wa Mazao Ya Biashara Na Chakula Kwa Wakulima.

Kwa Upande Wake Mkuu Wa Wilaya Ya Bukombe  Josephat Maganga Amewataka Wakulima Hao Kununua Mbegu Katika Makampuni  Yaliyoteuliwa  Na Serikali Ambayo Yanauza Mbegu Zenye Ubora Na Si Kwingineko Ambazo Zitakuwa Na Ubora Na Zenye Uwezo Wa Kuota Kwa Wepesi Zaidi.

Na Makunga Peter .
Share it:

habari

Post A Comment: