WAVAMIZI WA MISITU WAONDOLEWA BUKOMBE

Share it:
Baadhi ya miti ikiwa imekatwa katika moja kati ya mistu iliyopo Wilayani Bukombe.



Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wilayani Bukombe mkoani Geita Josephati Maganga  amepiga marufuku shughuli za kibinadamu zinazoendelea kufanyika katika msitu wa hifadhi  ya  biharamulo .

Maganga amesema kuwa baada  ya kutembelea ndani ya msitu huo kwa  wiki moja kwa ushirikiano na maafisa wa wakala wa mistu nchini  (TFS) wamefanikiwa kubaini uharibifu mkubwa wa msitu huo unaochangiwa na baadhi ya watu walioingia ndani ya msitu kinyume na sheria ya hifadhi za misitu namba 14 ya mwaka 2002.

“Hii sheria ya misitu imetoa makatazo inasema tusifanye mambo yafuatayo la kwanza tusifanye shughuli za kibinadamu ndani ya misitu, ulimaji unasabaibisha kukata miti, ukikata miti itaisha, malisho ya mifugo kwa hiyo Serikali inasema hapana kuingia kwenye misitu na kukata miti” alisisitiza Maganga.

katika hatua nyingine Maganga ameongoza kikosi cha kamati ya ulinzi na usalama wilaya, katika kuwaondoa wavamizi wa hifadhi hiyo na kufanikiwa kukamata zana haramu za uvunaji misitu, mifugo na kubomoa vibanda 214 vya makazi  ya watu.

kwa upande wake meneja wa wakala wa hifadhi za mistu wilayani humo  (TFS) Zacharia Kitare ameelezea  katika msitu wa hifadhi ya Kahama Biharamulo yenye jumla ya hekta mia moja thelathini na nne elfu na mianane sitini na nne 864 wilaya ya bukombe ina miliki  hekta elfu 14 pekee na kati ya hizo hekta elfu tatu  mia moja hamsini zimekwisha haribiwa na wanachi waliovamia   msitu  huo.

Imeandaliwa na Madukaoline.
Share it:

habari

Post A Comment: