MAADHIMISHO YA WIKI YA NENDA KWA USALAMA BARABARANI YAFUNGWA .

Share it:
Mkuu wa kikosi cha usalama barabarani Taifa Kamanda ,Mohammed Mpinga Akitoa taarifa ya wiki nzima ya nenda kwa usalama barababrani  wakati wa kufunga maadhimisho  hayo yaliyofanyika katika viwanja vya kalangalala vilivyoko mjini Geita.
Mgeni Rasmi Mkuu wa wilaya ya Geita,Herman Kapufi akisalimiana na baadhi ya wajumbe wa kamati ya usalama barabarani wakati alipokuwa amewasili katika viwanja vya Kalangalala.


Maandamano yakiwa yamepamba moto yakiingia katika viwanja vya kalangalala kwaajili ya kufatilia kile ambacho kilikuwa kikiendelea katika ufungaji wa wiki ya nenda kwa usalama.


Waendesha pikipiki maarufu kama boda boda wakipita  mbele ya mgeni Rasmi wakionesha kuwa nao wako makini katika kujali swala la usalama barabarani.

Mgeni Rasmi akitoa vyeti vya ushiriki wa jeshi la polisi .

Kikosi cha mpira cha polisi kikionesha kombe walilonyakua katika mashindano ya nenda kwa usalama yaliyofanyika wiki nzima.



MAADHIMISHO  ya wiki ya nenda kwa usalama barabarani Kitaifa yaliyokuwa yakifanyika Mkoani Geita yamefungwa rasmi leo,kwa kutoa elimu kwa makundi mbalimali ya kijamii ikiwa ni mkakati  wa Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama barabarani Kukabiliana na  ajali  ambazo zimekuwa zikigharimu maisha ya Watanzania kila mwaka.

Akitoa taarifa ya wiki nzima ya nenda kwa usalama barababrani mkuu wa kikosi cha usalama barabarani taifa Mohammed Mpinga wakati wa kufunga maadhimisho  hayo yaliyofanyika katika viwanja vya kalangalala vilivyoko mjini Geita.

Mpinga alisema makundi mbalimbali  yamenufaika katika Mkoa wa Geita wakiwemo wanafunzi wengi wa mkoa huo pamoja na jamii kwa ujumla huku waendesha bodaboda wakipewa kipaumbele kwani wao ndio wanasababisha ajali kwa wingi.

Awali mwakilishi wa Mkuu wa mkoa wa Geita ambaye ni mkuu wa wilaya ya Geita Herman Kapufi wakati wa Hotuba yake alisema ajali zinaweza kuepukika kama watu watafuata sheria na waendesha bodaboda kuvaa kofia ngumu pamoja na abiria wao wanapowabeba kwenda sehemu mbalimbali za mkao huo.

Katika hatua nyingine Mh Kapufi alisema  watahakikisha watu wote wanafuata sheria kwa kusoma na kuwa na leseni huku akiwaasa madereva wote wanaoingia na kutoka katika Mkoa huo kuwa na nidhamu wakati wa kuendesha vyombo vya moto.

 Baadhi  ya wananchi wameomba elimu ya usalama barabarani iendelee kutolewa kwa wananchi wote kila wakati kwani wengi wao hawana  uelewa  wa kutosha.

Maadhimisho  ya kitaifa ya wiki ya nenda kwa usalama barabarani yalifunguliwa Septemba  26 na Naibu waziri wa mambo ya ndani  Mhandisi Hamed Masauni katika viwanja vya kalangalala  na kufungwa leo na mwakilishi wa mkuu wa mkoa wa Geita na ujumbe wa mwaka huu wa maadhimisho ya wiki ya nenda kwa usalama unasema “hatutaki ajali tunataka kuishi salama”.





Share it:

habari

Post A Comment: