WANANCHI MKOANI GEITA WAMETAKIWA KUFUATA KANUNI NA TARATIBU ZA KUINGIA KATIKA MGODI WA DHAHABU WA GEITA GGM

Share it:
Eneo ambalo watu wamekuwa wakipenya kinyemera kuingia katika mgodi wa GGM,ambalo linaelezwa kuwa ni hatari kwa maisha ya wananchi ambao wamekuwa wakiingia bila ya kuwa na vibali.

Maelekezo yakitolewa na moja kati ya wataalam katika mgodi huo mbele ya waandishi wa habari wa Mkoani Geita.






Meneja mahusiano wa Mgodi wa GGM Tenga B Tenga akifafanua na kuonesha maeneo ambayo ni hatari kwa wananchi kuingia bila ya kuwa na kibali.

Eneo la mgodi wa GGM Kazi zikiendelea.


Wananchi  Mkoani Geita wametakiwa kufuata kanuni na taratibu Za Kuingia Katika Mgodi Wa Dhahabu Wa Geita  (GGM),Ili Kukabiliana Na Majanga  Ambayo Yanaweza Kujitokeza Ikiwa Ni Pamoja Na Kuingia Kwenye Mashimo Kwa Baadhi  Ya Wananchi Ambao  Wamekuwa Wakiingia Kinyemela  Katika Mgodi Huo.

Rai  hiyo imetolewa  na meneja  mahusiano wa GGM Tenga  B Tenga   Wakati alipokuwa akizungumza na mtandao wa madukaoline juu ya athari ambazo zinaweza kujitokeza endapo mtu akiingia mgodini hapo kinyemela bila ya kufuata taratibu zilizowekwa.

Aidha  Tenga,Amesema kuwa endapo mtu anaingia mgodini pasipokuwa na mavazi maalum ba bilaya ya kuwa na mwenyeji  kuna hatari ambazo zinaweza kutokea ni pamoja na kudumbukia katika mashimo ambayo yamekwisha kuchimbwa na mwisho wa siku kujikuta akiwa amejeruhika  hivyo ni vyema kwa mtu yoyote kuingi mgodini akiwa na kibari maalum kinachomruhusu.

Hata hivyo mtafiti  wa maswala ya miamba katika Mgodi wa dhahabu wa GGM Hatari Mjinja amefafanua  madhara yanayoweza kutokea Kutokana na miamba taka(mangwangala) ni uharibifu wa mazingira endapo kama hayatatengwa sehemu ambayo ni maalum.

CHANZO /MADUKA ONLINE


Share it:

habari

Post A Comment: