MGAMBO AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA TUHUMA ZA RUSHA

Share it:


Image result for MAHAKAMANI

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Wilaya ya Bukombe Mkoani Geita  imemfikisha mahakamani mgambo wa kata ya uyovu, tarafa ya Siloka wilaya ya humo, Bwana IDDI KIIGE NDUMIW kwa makosa mawili(2) ya kuomba na kupokea hongo kinyume na kifungu cha 15 cha Sheria ya Kuzuia Na Kupambana na Rushwa Na. 11 ya mwaka 2007.

Akisomewa makosa hayo mbele ya Hakimu Mkazi  wa Mahakama ya Wilaya ya Bukombe Mhe. VERONICA SELEMAN mwendesha mashtaka wa TAKUKURU Bi. HUSNA KIBOKO aliieleza  mahakama kwamba katika tarehe tofauti kati ya tarehe 29 mwezi wa 12 mwaka jana  na tarehe 3 mwezi wa kwanza mwaka huu Mshtakiwa akiwa mgambo alimkamata Bwana MAYUNGA NYERERE aliyekuwa amebeba magogo na kumuomba hongo ya kiasi cha shilingi elfu kumi(10,000/=) ili asiweze kumchukulia hatua za kisheria kwa kutoa taarifa Katika mamlaka husika.

 Aidha mshitakiwa alishawishi , kuomba na kupokea hongo ya kiasi cha shilingi elfu kumi(10,000/=) wakati akijua kwamba ni kosa kwa mujibu wa sheria ya Kuzuia Na Kupambana na Rushwa Na. 11 ya mwaka 2007.

Baada ya kusomewa mashitaka mshtakiwa amekana mashtaka yote dhidi yake, Mwendesha mashtaka ameiambia  Mahakama kuwa uchunguzi wa tuhuma hizo umekamilika na kuomba tarehe ambapo kesi yake itatajwa tena tarehe 18/mwezi huu kwa ajili ya kumsomea mshitakiwa maelezo ya awali.

Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Geita Bw. THOBIAS NDARO ametoa shukrani kwa raia wema wanaotoa ushirikiano kwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU).

Pia Amewataka wananchi kuwa na Uthubutu na kuendelea kutoa taarifa za vitendo vya Rushwa wakati wowote wanapohisi au kuona vinatendeka ili watuhumiwa waweze kuchukuliwa hatua za kisheria.




Share it:

habari

Post A Comment: