WANANCHI WAGOMA KUKUBALIANA NA MRADI WA BWAWA LA MAJI WA SH,MIL 74 MBELE YA NAIBU WAZIRI WA TAMISEMI

Share it:

Mwenyekiti wa Kasamwa,akimwelezea  Naibu waziri wa TAMISEMI  Seleman Jafo ,wakati alipotembelea Bwawa la kasamwa Wilayani Geita kujionea ujenzi ulivyo fanyika

Mkazi wa kasamwa Fabiani Maenge akimweleza Naibu waziri wa TAMISEMI  Seleman Jafo,namna fedha zilizotolewa ambavyo hazijaweza kuzaa matunda kutokana na Bwawa hilo kuendelea kuwa chafu.

Mhandisi wa maji wa halmashauri ya Mji wa Geita Gaspar Shoo,akielezea namna fedha hizo zilivyofanya kazi kwenye Bwawa la katoro.

Mbunge wa Geita vijijini ambaye pia ni Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi Joseph Kasheku(MSUKUMA)akifafanua  jambo wakati wa ziara ya  Naibu waziri wa TAMISEMI  Seleman Jafo

Makamu mwenyekiti wa halmashauri ya Mji wa Geita,Constatine Molandi akimweleza waziri namna ambavyo wamefanya mikakati ya kuweka sawa Bwawa hilo

Diwani wa kata ya Kasamwa,Mery Kasanda akifafanua namna ambavyo wameweza kujitaidi kuondoa kero ya kukosekana kwa maji katika kata yake.
Bwawa ambalo limekuwa likilalamikiwa na wananchi kwa muda mrefu.

Mbunge wa viti maalum Jimbo la Geita Upendo Peneza akitoa ufafanuzi juu ya kuhakikisha anafikisha kilio cha wananchi kwenye halmashauri ya mji wa Geita na kama itashindikana swala la Bwawa atalifikisha Bungeni.Hivi karibuni wakati alipofanya mkutano wa hadhara


Zikiwa ni siku chache tangu mbunge wa viti maalum kwa tiketi ya chama cha Demokrasia na maendeleo chadema Mkoani Geita Upendo Peneza kufanya mkutano  wa hadhara na Wananchi wa kata ya Kasamwa na kumwomba kushughulikia kero ya upatikanaji wa maji katika Bwawa la kasamwa hali hii imemlazimu  Naibu waziri wa ofisi ya Rais tawala za Mikoa na Serikali za mitaa TAMISEMI Bw.Suleiman Jafo kufika na kujionea ukarabati ulivyofanyika wa Bwawa hilo.


Katika hali isiyo ya kawaida wananchi wa Katoro wamegoma kukubaliana na taarifa ya Utekelezaji wa mradi wa Bwawa la Maji unaotajwa kutekelezwa kwa kiasi cha fedha Shilingi milioni 74 kwani fedha iliyotumika ni tofauti na ujenzi wa Bwalo hilo ulivyo kwasasa.

Hali hiyo imemlazimu Naibu waziri wa ofisi ya Rais tawala za Mikoa na Serikali za mitaa TAMISEMI .Suleiman Jafo aliyekuwa katika ziara ya siku moja wilayani Geita kuahidi kuunda Tume ya Uchaguzi itakayo toa taarifa kamili ndani ya wiki tatu

“Nitaunda tume maalum ya kuja kuchunguza mradi huu na kama fedha ambazo zimetolewa hazijafanywa kama inavyotakiwa tutawachukulia hatua za kisheria wale wote ambao wameusika katika ujenzi wa Bwawa hilo”alisema Jafo

Awali katika taarifa iliyotolewa na Mhandisi wa maji wa halmashauri ya Mji wa Geita Gaspar Shoo,imesema kuwa Mradi wa Bwawa unaohudumia wananchi wa kata za Kanyara na Kasamwa uligharimu Milioni 74


Ujio wa naibu waziri uliokuwa na agenda moja ya kuangalia changamoto za maji Mkoani Geita umekuja ikiwa ni sikuchache baada ya  Mbunge wa viti Maalum mkoani humo Kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo Bi.Upendo Peneza kumtaka kufika kuzungumza na wananchi na kutafuta suluhu ya tatizo

“Mimi kama Mbunge kazi yangu ni kuendelea kusema na kuwaelezea kero zenu Bungeni na kutokana na hali hii niwaakikishie sitachoka kufikisha kilio chenu cha uhaba wa maji kwa waziri mwenye dhamana na nitaakikisha waziri anafika kujionea wizi uliofanyika katika ujenzi wa Bwalo hili”Alisisitiza Upendo

IMEANDALIWA NA MADUKAONLINE

Share it:

habari

Post A Comment: