OJADACT YALAANI KITNEDO CHA MWANDISHI WA HABARI KUPOTEA KWENYE MAZINGIRA YA KUTATANISHA

Share it:
Image result for OJADACT



Chama  cha  Waandishi wa  Habari wa Kupiga  Vita  Matumizi  ya Dawa za Kulevya  na Uhalifu Tanzania(OJADACT), kimeungana na Waandishi  wa Habari, wadau  na wanafamilia wa Mwandishi wa Habari Bwana  Azory  Gwanda , anayefanya  kazi na  Mwananchi  Communications  Ltd  Mkoa wa Pwani, kulaani  tukio la kushikiliwa  kwake na  watu wasiojulikana, kuanzia Alhamis   Novemba 30, 2017  hadi  sasa.

Akizungumza na waandishi wa habari kwenye ofisi za chama hicho Mwenyekiti wa OJADACT   Bw,Edwin Soko amemwomba  Mkuu  wa  Jeshi la Polisi  Nchini Simon   Sirro,  kufuatilia  kwa  ukaribu  tukio  la kupotea  kwa Mwandishi huyo  na  kuhakikisha anapatikana  akiwa  salama, pia tunawaomba  watanzania kuwa watulivu wakati Jeshi la polisi  lkitekeleza  wajibu wake.

Soko ameongeza kuwa OJADACT  inaamini kwenye  kuheshimu  haki za binadamu kupitia   katiba  ya  Nchi,   Ibara ya  14 inaanisha kuwa, “kila mtu ana haki ya kuishi na kupata  toka kwa jamii  hifadhi ya maisha  yake, kwa mujibu wa sheria” Hivyo  kila mtu anastahili  kuishi na kuwa salama.

Pia ametoa rai kwa   wamiliki wa  Vyombo vya  Habari Nchini,  kuwa  na mifumo ya kisasa  ya ulinzi kwa Waandishi  wao, pamoja  na Mwandishi  mmoja  mmoja  kujifunza  mbinu za viashiria  hatari, (Security  alert  detection), ili  kujilinda.

Na kwamba chama hicho,  kinafuatilia  kwa  ukaribu suala  hilo kwa kushirikiana  na Vyombo vya ulinzi na usalama,  Kampuni ya  Mwananchi  Communications  LTD,  Wanahabari, na wadau  wote  wa  Habari Nchini kujua  kujua  mustabali wa Mwandishi Azory  Gwanda.
Share it:

habari

Post A Comment: