MRADI WA UONESHAJI WA FILAMU ZA MAZINGIRA BURE WAZINDULIWA MKOANI GEITA NA WAZIRI WA AFYA WA SERIKALI YA MAPINDUZI ZANZIBAR

Share it:
Waziri wa Afya, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Tamasha la Kimataifa la Filamu Zanzibar ZIFF, Mhe.Mahmood Thabith Kombo, akizungumza kwenye Uzinduzi wa Mradi wa Uoneshaji Filamu bure kwa njia ya Sinema mkoani Geita, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe.Nape Nnauye.
Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania, Bi.Joyce Fessoo, akizungumza kwa niaba ya Serikali kwenye uzinduzi huo ambapo aliwahakikishia Wanatasnia ya Filamu mkoani Geita na nchini kwa ujumla kwamba Serikali itahakikisha inaboresha zaidi sanaa ya filamu ikiwemo kuendelea kutoa mafunzo ya filamu kwa wanatasnia hiyo ili filamu zinazozalishwa ziwe na ubora
Mkuu wa Mkoa wa Geita, Meja Jenerali Mstaafu, Ezekiel Kyunga, akizungumza kwenye Uzinduzi wa Uoneshaji wa Filamu mkoani Geita, ambapo alisisitiza kwamba sanaa ni ajira hivyo wanatasnia hiyo watumie fursa mbalimbali ikiwemo mafunzo yanayotolewa na serikali ili kuboresha zaidi kazi zao.
Katibu wa Tamasha la Kimataifa la Filamu Zanzibar ZIFF, Robert Manondolo, akizungumza kwenye uzinduzi huo ambapo alibainisha kwamba ZIFF imekuwa ikitoa ufadhiri kwa taasisi mbalimbali nchini ikiwemo Taasisi ya Kijani Consult kwa lengo la kuziwezesha kufikisha elimu kwa umma kwa njia ya kuonesha filamu bure na kufikisha elimu iliyokusudiwa.

Mkuu wa idara ya Habari, Kijani Consult Tanzania, Rose Mweko, akitoa salamu zake kwenye uzinduzi wa mradi wa kuonesha filamu bure katika maeneo ya wazi mkoani Geita.

Katibu Tawala Wilayani Geita, Thomas Dimme, akizungumza kwenye uzinduzi wa Tamasha la Uoneshaji wa Filamu bure mkoani Geita ili kufikisha elimu mbalimbali ikiwemo Ufugaji na utunzaji wa Mazingira.




Uzinduzi huo ulifanyika jana katika Ukumbi wa Desire Park Geita ambapo Taasisi ya Sanaa Na Mazingira ya Kijani Consult Tanzania imeanzisha kampeni ya kuonesha bure Filamu mbalimbali kwa ajili ya kufikisha elimu kwa umma ikiwemo elimu ya Utunzaji wa Mazingira (Mabadiliko ya Tabianchi), Ufugaji wa kuku wa kienyeji, Usalama barabarani, Madawa ya kulevya, Madhara ya ndoa za utotoni miongoni mwa mambo mengi ya kijamii. Mradi huo umefadhiriwa na ZIFF.

Kutokana na Mwitikio wa wanatasnia ya Filamu mkoani Geita kuonesha shauku ya kuwa na Maonesho hayo ya Filamu, Mhe.Kombo alisema mwakani Tamasha la Kimataifa Zanzibar pia litafanyika mkoani Geita ikiwa ni sehemu ya ZIFF ni sehemu ya kusherehekea miaka 20 tangu kuanzishwa ZIFF.

Share it:

michezo

Post A Comment: