RAIS MAGUFULI ASITISHA UTOAJI WA LESENI ZA UCHIMBAJI MADINI

Share it:

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli ameiagiza Wizara ya Nishati na Madini kusitisha utoaji wa leseni mpya za uchimbaji halikadhalika leseni ambazo zimeisha muda wake.


Mhe. Rais Magufuli amezungumzia uamuzi wa Serikali kupeleka Miswada Mitatu ya dharura Bungeni kuwa unatokana na umuhimu wa hilo katika kutetea maslahi mapana ya nchi na kuhakikisha rasilimali za nchi zinawanufaisha wananchi.

Mhe. Rais Magufuli amewaonya wanachama wa Chama cha Mapinduzi CCM wenye nia ya kugombea nafasi mbalimbali katika Uchaguzi wa Chama hicho kutojihusisha na rushwa kwa vile rushwa ni adui wa haki, hivyo, atakayebainika kutumia rushwa atapoteza sifa ya kuwa Mgombea.

Akizungunzia ujenzi wa barabara ya kutoka Kamanga hadi Sengerama kwa kiwango cha lami, Mhe. Rais Dkt. Magufuli amesema kwa sasa Serikali imeshampata mkandarasi kwa ajili ya kufanya upembuzi yakinifu na usanifu ili barabara hiyo ianze kujengwa katika kutimiza ahadi aliyoitoa wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.

Rais Magufuli pia amewataka Wakuu wa Mikoa na Wilaya nchni kufafanua kwa wananchi na kusimamia uamuzi wa Serikali wa kufuta tozo zaidi ya 80 katika mazazo ya Kilimo, tozo 7 za Mifugo na tozo 5 za Uvuvi ambao lengo lake ni kuwaondolea kero wananchi.
Aidha, amesema Serikali inafanya uchambuzi ili kubaini wale wote waliotoa pembejeo hewa na atakayebainika atachukuliwa hatua kali za kisheria.

Wakati huo huo, Mheshimiwa Rais Magufuli ameiagiza Wizara ya Nishati na Madini kusitisha utoaji wa leseni mpya za uchimbaji na halikadhalika leseni ambazo zimeisha muda wake. Ametoa maagizo hayo alipokuwa akizungumza na wananchi wa Geita ambao walizuia msafara wake katika maeneo mbalimbali wakati akiwa njiani kuelekea Chato.

Jaffar Haniu
Naibu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Sengerema,Mwanza

04 Julai 2017.

Share it:

JOEL MADUKA

habari

Post A Comment:

Also Read

“SERIKALI AINA TATIZO NA SEKTA BINAFISI “NAIBU WAZIRI OLE NASHA

Naibu Waziri wa Elimu William Ole Nasha kizungumza kwenye mahafari ya Tatu ya shule za wavulana na wasichana za Sekond

JOEL MADUKA